Maumivu ya kukosa kile unachotakiwa kupata, kukosea, au kupata hasara ni somo ambalo linakusubiri wewe kujifunza. Katika kila maumivu unayopata, lipo somo la kutakiwa kujifunza na kulifanyia kazi.
Kwenye maisha huwezi kupata kitu bila sababu, hata maumivu unayoyapata si bure, ipo sababu ya wewe kujifunza kupitia maumivu hayo. Jiulize unajifunza nini kutokana na maumivu unayoyapata?
Inawezekana kwa sababu ya maumivu, unajifunza kutokana na makosa yako, au unajifunza kulinda thamani na mafanikio au chochote kile unajifunza. Jiweke huru na maumivu yako na kisha, amua kujifunza.

0 Comments