Fikiri kwenye maisha yako kama chochote unachokitaka kingekuwa kinapatikana kwa urahisi bila changamoto yoyote. Unafikiri maisha yangekuwaje?
Kwa mfano, kama unataka gari, ukifikiri tu umelipata, kama unataka nyumba ukifikiri tu unayo, kama unataka kusafiri, ukiwaza kufumba macho na kufumbua umefika, hebu waza unafikiri maisha yangekuwaje.?
Kwa bahati nzuri au mbaya haiko hivyo kwa sababu, thamani ya vitu imewekwa kwenye changamoto. Kama tungekuwa tunapata vitu bila changamoto, basi visingekuwa na thamani kabisa kwetu.
Tunathamini vile tulivyonavyo kwa sababu tumevihangaikia, kwa sababu vimetupa changamoto. Kama pasingekuwa na changamoto, basi tungepata kwa urahisi kweli na pia tungepoteza kwa urahisi sana.
Imeandikwa na Imani Ngwangwalu

0 Comments