BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

Mafanikio ni mchakato.

 

Unapokuwa umejiwekea malengo yako, acha kuwaza tu matokeo ya mwisho utakayopata, waza juu ya mchakato utakaokufikisha kwenye malengo yako.

Unatakiwa uelewe mchakato wa kuelekea kwenye malengo yako ni kama gari la kukufikisha kwenye malengo hayo. Unatakiwa kuufata mchakato kila siku, hadi ufanikiwe.

Unatakiwa kujua ili mchakato ukamilike, lazima uwe na juhudi na nidhamu. Hayo ni mambo mawili ya msingi ambayo yapo kwenye mchakato wa  ndoto zako ulizonazo.

Wengi wanachukia mchakato, badala ya kuufurahia. Jifunze kufurahia mchakato na habari ya matokeo yatakuwaje haikuhusu sana, wewe komaa na mchakato, matokeo yatakuja yenyewe.

Wako rafiki katika mafanikio ; Imani Ngwangwalu

Bonyeza hapa kuwasiliana nami kupitia E-mail

dirayamafanikio@gmail.com

BONYEZA HAPA http://wa.me/255687449428 ili kuwasiliana na Imani Ngwangwalu kupitia WhatsApp.


Post a Comment

0 Comments