Ikiwa unataka kufanikiwa katika jambo fulani basi hakikisha ya kwamba unawekeza nguvu, akili na uwezo wako katika jambo ambalo wewe mwenyewe unahisi jambo hilo ni bora zaidi kwako.
Ikiwa nguvu, akili na uwezo wako unao uwezo wa kufanya vizuri zaidi katika mpira wa miguu basi wekeza muda wako mwingi sana katika kujiimarisha katika jambo hilo.
Si katika mpira pekee bali fanya uchunguzi wa kujinguza ili kujua wewe upo vizuri katika jambo gani kasha wekeza muda wako mwingi katika kujiimarisha katika eneo hilo ili uweze kufanya na kuleta matokeo yenye tija.
Kuendelea kufanya jambo ambalo si la kwako huko ni kupoteza muda mwingi pasipo kuwa na sababu za msingi, Hii ni kwa sababu tunaamini kila mwanadamu ameubwa na uwezo wako binafsi katika kukamilisha jambo fulani hivyo kila wakati ni lazima namna ya kuwa bora katika jambo hilo.
Ndimi:
Afisa Mipango, Benson Chonya.
Bonyeza
hapa kuwasiliana nami kupitia E-mail
BONYEZA HAPA https://wa.me/255747030303 kuwasiliana nami kupitia WhatsApp.

0 Comments