Watu wengi wameshindwa kufanikiwa kwa viwango vya hali ya juu kwa sababu ya wengi wao wanashindwa kuweka umakini kwenye mambo wayafanyayo. Wengi wao wamekuwa ni watu wakuchanganya mambo mbalimbali ya msingi kwa wakati mmoja.
Kitendo hiki kisaikolojia tunakiita si cha kiungwana kwa sababu akili nayo inakuwa inashindwa kuweka umakini kwenye jambo moja. Hata wahenga nao walisema mshika mbili, moja mponyoka.
Hivyo ikiwa unataka kufanikiwa katika jambo fulani ulifanyalo kwa viwango vya juu ni wakati wako kuhakikisha ya kwamba unakamilisha jambo moja kwa ufasaha kabla ya kuanza kufanya jambo jingine.
Ndimi:
Afisa Mipango, Benson Chonya.
Bonyeza
hapa kuwasiliana nami kupitia E-mail
BONYEZA HAPA https://wa.me/255747030303 kuwasiliana nami kupitia WhatsApp.

0 Comments