Ukishaona tayari umechukua uamuzi wa kufanya jambo fulani, unachotakiwa kufanya kuchukua hatua kwa haraka sana. Inawezekana hatua hizo zisiwe kamili, lakini kuchukua hatua ni kitu cha muhimu sana.
Na unapochukua hatua kwa haraka, inakusaidia kukuhamasisha kwenda mbele zaidi na kukuondolea wasiwasi na kukata tamaa mapema. Ni rahisi sana kufanya, kama utachukua hatua mara moja.
Unapochukua uamuzi wa kufanya jambo lako, chukua hatua mara moja, ukichelewa kuchukua hatua, upo uwezekano, hutafanya kabisa. Jiulize, ni mara ngapi hujafanya kabisa jambo lako, mara baada ya kuchelewa kuchukua hatua?
Imani Ngwangwalu.
0 Comments