BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

NAMNA YA KUTENGENEZA VILEJA

 

Mahitaji

1.      Siagi 1 cup

2.      Sukari 1 cup

3.      Mayai 2

4.      Unga wa ngano  vikombe 4

5.      Baking powder 1 tsp

6.      Arki(essence) unayopenda 1 tbsp ..nimetumia arki ya banana

Saga sukari na siagi mpaka ichanganyike vizuri, tia yai 1 zima , la pili tia kiini tu , ute weka pembeni ,endelea kusaga kwa dakika 1 mpaka 2 ,weka baking powder na arki/essence, saga tena kidogo anza kutia unga wa ngano kidogo kidogo mpaka unga unashikana linakua donge gumu la kiasi ,nimetumia unga vikombe 4, Ila muhimu angalia donge lishikane kiasi . Weka sehemu kama kibao cha kukatia maandazi ,usukume unga kama chapati Ila usiwe mwembamba sana,tumia kitu chochote kukata(unaweza kufanya shape unayopenda) nimetumia glass kukatia. Ukimaliza zote kuzikata ziweke kwenye trey upake ule ute wa  yai juu ,bake mpaka vinawiva,.. vitoe

Iyo ya juu ni chocolate, yayusha milk chocolate na maziwa au double cream then tia kwenye piping bag au kitu chochote ambacho itatoka nyembamba uchoree juu . Sio Lazima uweke chocolate juu.

Nimetumia arki ya banana ambayo ilileta rangi hiyo ,ukitumia arki nyengine mfano vanilla inaweza kutokea rangi tofauti kidg Ila haina tatizo.

Imeandikwa na Afisa Mipango Benson Chonya kwa msaada wa mtandao.


Post a Comment

0 Comments