1. Karanga Kilo 5
2.
Sukari vikombe 2
3.
Maji vikombe 1
4.
Maziwa ya unga 2 vijiko vya chai
Namna
Ya Kutayarisha Na Kupika
1. Saga karanga zilizokaangwa na kumenywa mpaka
zilainike kiasi.
2. Kisha changanya maji na sukari weka jikoni
yachemke mpaka yanate kidogo kama shira. Changanya unga wa karanga na maziwa ya
unga kisha mimina kwenye hiyo shira.
3. Koroga taratibu kwa moto mdogo mpaka uone
imeshikana na inanata.
4. Paka mafuta treya kisha mimina na utandaze upesi upesi.
5. Acha ipoe kidogo tu kisha katakata vipande
na acha ipoe kabisa.
Imeandikwa na Afisa Mipango Benson Chonya kwa msaada wa
mtandao.
0 Comments