BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

JINSI YA KUTENGENEZA TOMATO SOURCE.



Yafuatayo ndiyo mahitaji ya kutengeneza tomato source.

1. Nyanya kilo 1.

2. Vitunguu maji viwili.

3. Vinegar vijiko 3 vya chai.

4. Sukari vijiko 2 vya chai.

5. Chumvi kijiko kimoja cha chai

6. Maji ya moto kikombe kimoja cha chai.

7. Mafuta ya kula vijiko 7 ya vyakula.


Haya ndiyo mahitaji ya kutaka kutengeneza tomato souce, hata hivyo kama unataka kutengeneza zaidi ya hapo unatakiwa kuongeza uwiano wa mahitaji hayo.


HATUA YA KWANZA.

A) Menya nyanya na vitunguu kisha vikate vipande vidogo vidogo.

B) Tumia Brenda kusaga mchanganyiko wako.

C) Anza kuweka malighafi namba 1 hadi namba 4 katika brenda yako kutokana na ratio (uwiano ) uliopewa hapo juu. Saga kwa dakika kadhaa hadi uone imetokea rojo laini.

HATUA YA PILI.

A) Tumia sufuria yenye nafasi kupika mseto huu.

B) Weka sufuria yako jikoni tia mafuta ya kula acha yachemke kisha mwagia mseto wako na kisha uanze kukoroga kwa dakika 30 kuelekea upande mmoja huku ukichemka.

C) Baada ya hapo epua mseto huo utakuwa tayari imeshakuwa tomato funga vizuri na kisha peleka sokoni.

Imeandikwa na Afisa Mipango Benson Chonya kwa msaada wa mtandao.


Post a Comment

0 Comments