Siku ya Wanawake ilianza kuazimishwa mwanzoni mwa miaka ya 1900. Ambapo wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani walioandamana kupinga mazingira duni ya kufanya kazi zao, walilalamikia ukosefu wa huduma za kijamii na kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji katika ajira. Kutokana na hali hiyo, nchi ya Marekani ilikubali kuwa na siku ya maadhimisho ya kitaifa ili kutafakari masuala mbalimbali yanayohusu haki na ustawi wa wanawake.
Tanzania ilianza kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani mwaka 1996, ambapo tumeona na tunazidi kushuhudia ya kwamba watu wanazidi kupata uelewa mpana juu ya siku hii ya wanawake duniani, kwani hapo zamani mwanamke alikuwa akitengwa katika kutoa maamuzi, hata katika usawa wa kupata elimu.
Lakini hivi sasa watu wamezidi kutambua mchango na thamani ya mwanamke katika jamii, kwani kila palipo na mafanikio yeyote yale nyuma yake yupo mwanamke. Hivyo kwa namna moja ama nyingine tuiheshimu siku hii kwa kutambua mchango wakina mama.
*********Asante Mama*********
By Afisa Mipango Benson Chonya

0 Comments