BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

Wanaume tuwafundishe wake zetu jambo hilo kwa manufaa ya familia.

Miongoni mwa mambo ambayo huwa yananishangaza mbele ya macho yangu na maskio yako ni pamoja na kuona na kusiakia eti kwa sababu amabazo siyo za msingi au wakati mwingine ikiwa ni wivu tu, wapo baadhi ya  wanaume wengi  huwa hawaruhusu wake zao kujishughulisha na kazi yeyote ile  ya kuingiza kipato na kuwafanya wake zao hao kuwa ni wakina mama wa nyumbani.

Mimi binafsi huwa nashindwa kuelewa kwa nini wapo wanaume wenye tabia kama hizo? Kwa sababu kama ambavyo wahenga waliwahi  kusema “hakuna aijuaye kesho” hivyo yawezekana leo wewe mwanaume u mzima wa afya tele na wewe ndiyo kila kitu kwenye ndoa hiyo kwa maana wewe ndiyo mtegemezi wa kiuchumi kwenye familia yako ya  ndoa.

Sasa itakuwaje endapo utaumwa ghafla na hautakuwa na uhakika wa kuitegemeza tena familia yako? Na ili hali hapo awali hukurusu mkeo  awe na shughuli ya kufanya ambayo ikingekuwa ni chanzo cha kutoteteleka kiuchumi hasa pale wewe ukiwa huna uwezo tena wa kufanya kazi?

Nadhani katika hili basi kwa kila mwanaume kwa nafasi yake basi ajitafakari na aone ni kwa namna gani ambapo kila mmoja wetu anapaswa kuliangalia hili kwa namna ya tofauti na kuona ni kwa namna gani mke wake badala ya kuwa ni mama wa nyumbani basi amruhusumama mkewe aweze kuwa shughuli ya kufanya ambayo itakuwa inaiingiza kipato badala ya kukaa na kusubiri mume peke ake awe ndiyo chanzo pekee cha kipato katika familia.

Wapo baadhi ya wanaume wanashindwa kuwaruhusu wake zao kujihusisha na shughuri mbambali eti kwa sababu wanaona wake zao watakuwa wahuni, Pia nikukumbushe ewe mwanaume ya kuwa unaposema mkeo akijihusisha na shughuri fulani basi utakuwa ni mwanzo wa yeye kuwa mhuni, kitu hicho siyo kweli kwa sababu uhuni ni tabia kama mkeo ni mhuni basi hata akikaaa nyumbani ni lazima atafanya uhuni tu.

Naomba nirudie tena kwa kusema ya kwamba hakuna aijuaye kesho hivyo nadhani itakuwa jambo la busara sana ewe mwanaume kuweza kumruhusu mkeo ajihusishe na kufanya kazi na si kuwa mama wa nyumbani.

Ndimi Afisa Mipango; Benson Chonya

mafanikioapp@gmail.com

0747030303

Post a Comment

0 Comments