BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

Kauli ambazo ni sumu kwenye mahusiano.

 


Mara nyingi tunapokuwa kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi basi tunapaswa kuwa makini sna na kauli ambazo tunazitoa kwa wenzi wetu kwani zina uwezo ukubwa sana wa kuyavunja mahusiano hayo.

Kauli hizo mara nyingi huwa zinaanzia kwenye matamshi yetu ambayo tunayosema na wakati mwingine mpaka kwenye yale tunayochati na wenzi wetu.

Kwa mfano unaweza ukakuta mtu yupo kwenye mahusiano, kwa kuwa mpenzi wake amemuudhi basi anadiliki kumwambia mpenzi wake wewe huna akili kabisa, mambo yako kama mtoto mdogo, kwanza nipo na wewe basi tu, au anamtukana matusi makubwa ambayo siwezi kuyaandika hapa au wakati mwingine kumfananisha na wanyama kama mbwa, paka na wanyama wengineo.

Matamshi kama haya kwa yule ambaye anayatamka huwa anaona yupo sahihi ila linapokuja kwa upande wa mtukwanaji ni kitu ambacho huwa kinapokelewa katika mtazamo ambao siyo chanya na wakati mwingi humuathiri kisaikolojia mtukwanaji huyo.

Wakati mwingine mtukwanaji huyo huwa anawaza mengi kwamba hivi mimi ni kweli ndivyo nilivyo? Hivi thamani yangu kwa mtu huyu ipo wapi? Mwisho wa siku mtukwanaji huyo anajenga visilani visivyokuwa na maana, ambavyo hupelekea mwisho wa siku kuvunjika kwa mahusioano hayo.

Binafsi naelewa kuwa chanzo cha matusi ya namna hiyo hutokana  na hasira kutoka kwa mtu aliyeudhiwa na mpenzi wake.

Hata hivyo haijalishi umeumia kiasi gani bada ya kuudhiwa na mwenzi wako nadhani litakuwa ni jambo la busara sana kutafuta namna sahihi ya kuongea na aliyekuudhi na si kumtukana na kumtakia maneno yasiyofaa kwani yana athari sana katika mahusiano yenu.

Hivyo niweke nukta  kwa sema “ukitaka kujenga mahusiano yako ya kimapenzi yaliyo bora zaidi basi jitahidi sana kila wakati kumtamkia mwenza wako yale yatakayomjenga na si yatakayosababisha kuvunjika kwa muhusiano yenu”

Ndimi Afisa Mipango: Benson Chonya

mafanikioapp@gmail.com

0747-030303

Post a Comment

0 Comments