Tafuta majibu ya changamoto |
Kuna wakati katika maisha
umekuwa ukisubiri baadhi ya mambo yakae sawa ndipo uanze kufanya jambo fulani. Lakini ukweli ni kwamba kufanya hivi ni sawa na
kusubiri jua lizame nyakati asubuhi, hii ikiwa na maana ya kwamba kusubiri muda
fulani ndiyo uanze mpango Fulani ni kujiadanganya mwenyewe.
Kwani unavyozidi
kusubiri, muda nao haukusubiri wewe na pia changamoto juu ya jambo hilo ndivyo
zinavyozid kuwa nyingi, hivyo kila wakati ni vyema kujitoa kwa kufanya jambo
ambalo una maksudi mazima ya kulitenda jambo hilo.
Hivyo ila wakati ni vyema
ukapambana na mambo magumu, wakati mambo
hayo bado ni rahisi. Vile vile pambana na changamoto zako, wakati changamoto
hizo bado ni kidogo. Pambana na kuitunza afya yako, wakati bado umzima. Pambana
na umaskini, wakati bado ukijana mwenye nguvu. Kwani upo usemi usemao
usipoitesa akili yako angali u kijana, basi jiandae kuutesa mwili wako pindi
utakapozeeka.
Usemi huo ni wa kweli kwa
sababu ila changamoto unayokutana nayo kwenye maisha, unaweza kuishinda ikiwa
utakabiliana nayo mapema. Acha kusubiri mambo yameharibika ndio uanze kukomaa
na changamoto yako. Acha kusubiri nyumba imeungua ndio utafute maji ya kuzimia
moto, au usubiri ufa ubomoe ukuta ndipo uanze kujilamu. Kafanya hivi ni sawa na
kuzima moto kwa kupiga chafya.
Hivyo kila wakati na kila
saa ogopa kuishi maisha ya zima moto. Ishi kwa mipango sahihi, ambayo mipango
hiyo mwisho wa siku itakuongoza wewe kuweza kufikia katika mafanikio yako
makubwa. Wengi wanashindwa katika maisha kwa sababu ya kuchelewa kuthibiti
mambo ambayo walitakiwa wayathibiti mwanzoni.
Labda tu Jiulize kwa
pamoja ni mara ngapi umekwama, kwa sababu ya kushindwa kuithibiti hali fulani
ambayo ulitakiwa kuithibiti mapema? Acha kuendelea kuharibu maisha yako kwa
kusubiri eti mpaka mambo yameharibika ndio utafute dawa yake. Changamka sasa na
anza kutekeleza majukumu yako mapema.
Hivyo kila nyakati ni
vyema ukatambua namna ya kutafuta majibu
mapema kwa kila changamoto ambayo inakukabili. Kwani kama endapo utaamua kukaa
kimya bila kutafuta majibu ya changamoto
ambayo inakukabili utakuwa katika hali ambayo kiukweli utakosa mtu wa kumlaumu
hapo baadae.
Hivyo ili kuepuka mtu wa
kumlaumu, ni vyema ukijiweka utarataibu wa kutafuta majibu ya changamoto zinazokukabili
mapema, itakusaidia wewe kuwa ni sehemu majibu ya changamoto hiyo. Lakini pia
pindi ujiwekeapo utaratibu wa kutafuta majibu ya changamoto mapema itakusaidia
wewe kuweza kulifanya jambo hilo kabla halijaharibika kwa kiwango kikubwa.
Hivyo tuagane na wewe
siku ya leo kwa sema ya kwamba “Endapo wewe ni mfanyakazi wa maofsini,
mfanyabiashara, mjasiliamali au ni mwanafunzi kuna mahali unapaona kabisa
kwamba mambo hayaendi sawa naomba ujiulize swali hili kila wakati, hivi ni wapi
ambapo huwa nakosea mpaka inakuwa hivi?
Imeandikwa na
uongozi wa mtandao wa dira ya mafanikio
Imani Ngwangwalu & Benson Chonya
0 Comments