Maisha ya mafanikio yanaundwa na vitu vidogo vidogo sana. Zile hatua ndogo kabisa ambazo unaziona haziwezi kukusaidia kufanikiwa, hizo ndizo zinaweza kukupa mafanikio kama utafanya kwa muda mrefu.
Hebu kama kuna kitu unataka kukifanya, anza kukifanya bila kujiuliza uliza. Acha kabisa kuahirisha mambo yako, utakuja kujuta sana baadae utakuwa umepoteza pesa nyingi na mafanikio kwa ujumla kwa sababu ya kuahirisha.
Ipo gharama kubwa sana ya kusubiri subiri na kuahirisha mambo kuliko unavyofikiri. Utapoteza mambo mengi sana ambayo moyo wako utakuuma sana na kujiuliza kwa nini ulisubiri na hujufanya mapema. Fanya na acha tena kusubiria kitu au kuahirisha.
0 Comments