BREAKING ARTICLES

6/recent/ticker-posts

NAMNA YA KUTENGENEZA TAMBI ZA DENGU.

 


Mahitaji:

1.      Unga wa dengu ½ kilo

2.      Unga wa pilipili binzari nyembamba ½ kijiko cha mezani

3.      Unga wa pilipili manga kijiko 1 cha chai

4.      Unga wa mchele ¼ kilo

5.      Chumvi kiasi

6.      Mafuta ya alizeti ½ lita

7.      Baking powder

Namna ya kutengeneza

Changanya unga wa mchele pamoja na ule wa dengu. Kisha chukua nyunyuzia baking powder na baadaye chumvi. Weka unga wa binzari nyembamba na pilipili manga. Changaya vizuri na kisha weka maji kidogo kidogo huku ukukanda hadi liwe donge gumu kama unavyofanya kwenye maandazi. Baada ya hapo weka donge lako pembeni na funika. Acha likae kwa muda wa nusu saa hadi saa moja.

Baada ya hapo chukua karai la mafuta weka jikoni acha hadi mafuta yapate moto kabisa. Kisha chukua mashine ya kupikia tambi na weka donge lako. Kandamiza taratibu huku ukiruhusu minyororo ya tambi kuingia kwenye mafuta yaliyo jikoni. Weka kiasi kiasi huku ukikaanga. Acha mpaka zitakapokuwa zimeiva na kukauka vizuri. Ipua na weka pembeni. Weka kwenye sahani safi na kavu. Tambi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Ikiwa huna mashine, unaweza kutumia bakuli ya bati iliyotobolewa mfano wa chujio. Na kisha kandamiza kwenye tundu hizo hadi unga wako upite kwenye tundu za bati hilo na kufanya kama nyuzi nene na ndefu. Fanya kama nilivyoelekeza hapo juu.

Imeandikwa na Afisa Mipango Benson Chonya kwa msaada wa mtandao.


Post a Comment

0 Comments