Acha kuridhika na kuona sawa tu, pale wanaposhindwa wengine. Jifunze kitu kutoka kwenye kushindwa kwao.
Acha kuumia na mafanikio ya wengine, bali jifunze wamefanya nini cha ziada hadi kikawafikisha hapo leo walipo.
Jifunze kutokana na mafanikio yako, jifunze kutokana na kushindwa kwako, amua kujifunza katika kila hali ya maisha unayopitia.
Maisha yana mambo mengi ya kujifunza, jambo la msingi kwako ni kuamua kujifunza kweli na kuchukua hatua mapema zitakazo kusaidia kufanikiwa.
0 Comments